Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 603 2023-06-13

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaongeza madaktari na watumishi wa kada nyingine katika Kituo cha Afya Mrijo chenye Daktari na Nesi mmoja?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ilipata kibali cha ajira na kuajiri Watumishi wa Kada ya Afya 7,340 ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ilipatiwa Watumishi 87. Kati ya hao, Watumishi wawili walipelekwa kwenye Kituo cha Afya Mrijo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imeajiri Watumishi wa Kada za Afya 8,000, ambapo Halmashauri ya Wilaya Chemba nayo imepatiwa Watumishi wa Afya ambao watapelekwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.