Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 604 2023-06-13

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatenga fedha za ukarabati wa madarasa, nyumba za Walimu na vyoo katika Shule za Msingi, Jimbo la Mbinga Mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jonas William Mbunda, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya tathmini ya hali ya uchakavu wa miundombinu katika Shule za Msingi Nchini na kubaini uwepo wa miundombinu inayohitaji ukarabati mkubwa, ukarabati mdogo, kubomoa na kujenga upya na isiyohitaji ukarabati. Kwa kuanzia mwaka wa fedha 2023/2024 kipaumbele kitakuwa ujenzi wa vyumba vya madarasa na shule mpya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu hali ya uchakavu kwa nyumba za Walimu, ni jukumu la Halmashauri kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika kukarabati nyumba za Walimu zilizopo kwenye maeneo yao na kuzitengea bajeti ili zikarabatiwe. Nitumie fursa hii kuwaelekeza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kufanya tathmini ya ukarabati wa nyumba za Walimu na kuchukua hatua stahiki.