Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha za ukarabati wa madarasa, nyumba za Walimu na vyoo katika Shule za Msingi, Jimbo la Mbinga Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Naomba nichukue nafasi hii kuishukuru Serikali kwa jinsi inavyoweka mikakati mizuri ya kufanya ukarabati wa miundombinu katika shule zetu za msingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mbinga Mjini lina Kata 19 na Kata nane ziko mjini, Kata 11 ziko vijijini lakini bado kuna changamoto kubwa sana ya Walimu katika eneo hili la Jimbo la Mbinga Mjini. Katika mgao wa Walimu ambao wameajiriwa hivi karibuni Jimbo la Mbinga Mjini halijapata Mwalimu hata mmoja. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba inamaliza changamoto hii katika Jimbo la Mbinga Mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie nafasi hii kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kumwelekeza Katibu Tawala, Mkoa wa Ruvuma kuhakikisha anafanya msawazo ndani ya Mkoa wake kwa maeneo ambayo yana upungufu wa watumishi. Kuna maeneo ambayo yatakuwa na watumishi au Walimu wengi zaidi na yale ambayo bado hayajapata watumishi, basi Katibu Tawala wa Mkoa aweze kuhakikisha anapeleka watumishi ikiwemo katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunda la Mbinga Mjini.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha za ukarabati wa madarasa, nyumba za Walimu na vyoo katika Shule za Msingi, Jimbo la Mbinga Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Jimbo la Manyoni Mashariki, Shule ya Msingi ya Iseke, Makanda na Sasagila ni kongwe sana. Je, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba wanapeleka madarasa kwenye hizi shule kongwe? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pius Chaya, Mbunge wa Manyoni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu hili lini Serikali itapeleka fedha katika shule hizi kongwe. Tayari Serikali kupitia mradi wa BOOST imetenga zaidi ya bilioni 230 kote nchini kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa shule kongwe hapa nchini na shule mpya katika halmashauri mbalimbali ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni. Hizi shule za Iseke, Makanda na Sasajira nazo tutazifanyia tathmini kuona uhitaji uliopo na baada ya hapo tutaziweka katika mipango yetu kwa ajili ya ofisi kutoa fedha.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha za ukarabati wa madarasa, nyumba za Walimu na vyoo katika Shule za Msingi, Jimbo la Mbinga Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Moja ya sababu za kushuka kwa ufaulu katika maeneo ya vijijini hasa Mbulu Vijijini ni kukosekana kwa nyumba za walimu na sisi tumejenga maboma yamefikia hatua mbalimbali.

Je, ni lini uko tayari kupeleka fedha katika majengo hayo? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei la nyumba hizi za walimu zilizojengwa kwa nguvu za wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Ofisi ya Rais, TAMISEMI, inafanya tathmini ya maboma yote ya nyumba za walimu ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi na pale tathmini hii itakapokamilika basi itawasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI na tutaiwekea katika mipango yetu kwa ajili ya utafutaji wa fedha ya ukamilishaji wa nyumba hizi.

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha za ukarabati wa madarasa, nyumba za Walimu na vyoo katika Shule za Msingi, Jimbo la Mbinga Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu lakini pia na swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Jimbo la Busega wamejenga maboma ya madarasa 69 na nyumba za walimu 11. Je, Serikali sasa iko tayari kupelekea fedha kwa ajili ya kumalizia maboma ya wananchi? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala hili la maboma kama nilivyotoka kusema hapa awali, tayari kuna timu kutoka Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa maelekezo yake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Angellah Kairuki ambayo inafanya tathmini kujua maboma ya nyumba za walimu lakini vilevile maboma ya madarasa, pale tutakapopata idadi kamili kutoka kwenye Halmashauri hizi ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Busega tukaa na kutafuta fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma haya. (Makofi)

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha za ukarabati wa madarasa, nyumba za Walimu na vyoo katika Shule za Msingi, Jimbo la Mbinga Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, Shule ya Msingi Mshizii, Mategho na Mavului zina hali mbaya sana. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kupeleka pesa kwa ajili ya ukarabati wa shule hizo? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue nafasi hii kumuelekeza Afisa Elimu wa Mkoa wa Tanga kufika katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto na kufanya tathmini katika shule ambayo ameitaja Mheshimiwa Shekilindi na tathmini hiyo ikikamilika basi wawasilishe Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kuona namna gani tunatafuta fedha katika mwaka wa fedha unaofuata kwa ajili ya ujenzi wa maboma hayo katika shule hiyo.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha za ukarabati wa madarasa, nyumba za Walimu na vyoo katika Shule za Msingi, Jimbo la Mbinga Mjini?

Supplementary Question 6

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Shule ya Sekondari Mpandapanda katika Wilaya ya Rungwe, Kata ya Kiwila ina wanafunzi wengi sana lakini ina idadi ndogo sana ya matundu ya vyoo. Ni lini Serikali itaongeza nguvu kuweza kujenga vyoo kwa ajili ya kuweza kuwasaidia wanafunzi hao? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la matundu ya vyoo katika shule hii ya Mpandapanda Wilayani Rungwe, ni Mkurugenzi wa Halmashauri sasa nae aweze kuangalia katika mapato yake ya ndani, atenge fedha kwa ajili ya kujenga matundu ya vyoo katika shule hii ambayo ina upungufu wa matundu hayo ya vyoo. Vilevile tutakaa na Mheshimiwa Mbunge tuweze kupata taarifa zaidi ya shule hii nakuona namna gani Serikali Kuu inaweza ikachangia.