Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 605 2023-06-13

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:-

Je, nini mpango wa kuajiri waganga, watumishi wa afya na kupeleka vifaatiba kwenye zahanati na vituo vya afya nchini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutoa vibali vya ajira kwa watumishi wa kada ya afya ili kupunguza uhaba wa watumishi uliopo. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Ofisi ya Rais, TAMISEMI, iliajiri watumishi 7,732. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 tayari Serikali imeajiri watumishi 5,319 wa kada za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni 69.95 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba. Kati ya hizo, shilingi bilioni 7.1 ni kwa ajili ya hospitali 71 za Halmashauri, shilingi bilioni 47.7 ni kwa ajili ya vituo vya afya 159 na shilingi bilioni 15 ni kwa ajili ya zahanati 300. Hadi kufikia mwezi Aprili 2023 jumla ya shilingi bilioni 58.85 zilikuwa tayari zimetolewa na Wizara ya Fedha na Mipango kwa ajili ya vifaatiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 116.92 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali.