Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je, nini mpango wa kuajiri waganga, watumishi wa afya na kupeleka vifaatiba kwenye zahanati na vituo vya afya nchini?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaishukuru sana Serikali kwa kuendelea kujenga vituo vya afya na vingine vile zamani kukarabatiwa lakini ningependa kujua ni lini Serikali sasa itapeleka vifaatiba vya kutosha katika Vituo vya Afya vya Hedaru, Kisiwani, Makanya, Ruvu na Shengena?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; zahanati nyingi katika Jimbo la Same Magharibi hususan katika Tarafa ya Mwembembaga, Chemesuji na Same, zahanati zimekamilika lakini hazina watumishi. Je, ni lini Serikali sasa itapeleka watumishi wa kutosha na waganga katika zahanati hizo ili wananchi waweze kupata huduma?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Dkt. David Mathayo David.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuhusu upatikanaji wa vifaatiba katika Jimbo la Same Magharibi. Niseme tu kwamba Serikali tayari imetenga shilingi milioni 300 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba katika vituo vya afya vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Same. Vilevile, shilingi milioni 100 kwa ajili ya zahanati zilizokuwepo katika Halmashauri ya Wilaya ya Same katika Mwaka wa Fedha wa 2023/2024. Hivyo nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge kwamba pale ambapo tutaanza utekelezaji wa bajeti mpya kwenye mwaka wa fedha unaokuja, tutaweka kipaumbele hizi fedha ziweze kwenda haraka kwa ajili ya ununuzi wa vifaa hivi tiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili la zahanati hizi kukosa watumishi kule Halmashauri ya Wilaya ya Same. Serikali imeajiri watumishi wa afya zaidi ya 8,070 katika mwaka huu wa fedha ambao tupo na tunaenda kuumalizia. Tutaangalia ni wangapi ambao wamepangiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Same ili zahanati hizi nazo Mkurugenzi nae aweze kufanya allocation ya hawa watumishi wapya watakaokwenda kwenye zahanati alizozitaja Mheshimiwa Mathayo.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je, nini mpango wa kuajiri waganga, watumishi wa afya na kupeleka vifaatiba kwenye zahanati na vituo vya afya nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Tunaishukuru Serikali kwa kujenga vituo vya afya katika Mkoa wa Manyara. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka wataalam wa kutosha pamoja na vifaatiba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ni commitment ya Serikali hii ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kwamba ina wataalam wa kutosha wa afya, ndiyo maana hivi karibuni Serikali ilitoa ajira 8,070 kwa wataalamu wa afya kote nchini na Mkoa wa Manyara nao wamepata mgao wao wa wataalam hawa wa afya.