Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 606 2023-06-13

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Shule ya Wasichana Arusha ambayo ilipangwa kujengwa katika Kata ya Enkikret - Longido?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia mradi wa kuboresha elimu ya sekondari imedhamiria kujenga shule za sekondari 26 za bweni za wasichana wanaosoma masomo ya sayansi kidato cha kwanza mpaka cha sita ambapo kila mkoa utajengewa shule moja. Ujenzi wa shule za bweni za wasichana za Mikoa unafanyika kwa awamu. Katika Awamu ya kwanza ya ujenzi Mikoa 10 imenufaika ambapo kiasi cha shilingi bilioni 30 zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa shule hizo na ujenzi upo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kuwa ujenzi wa Shule ya Mkoa wa Arusha utafanyika katika awamu inayofuata hivyo ombi lake lipo kwenye utaratibu wa utekelezaji, wakati wowote fedha zitakapokuwa tayari, zitapelekwa Halmashauri husika kwa ajili ya kuanza ujenzi huo.