Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Shule ya Wasichana Arusha ambayo ilipangwa kujengwa katika Kata ya Enkikret - Longido?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri lakini wananchi wa Longido wana hamu sana na shule hii, hadi sasa wako tayari kujitolea kwa nguvu kazi zao wenyewe ili basi kuendeleza shule hii. Je, Serikali haioni haja kuwapa kipaumbele wananchi hawa ambao wako site tayari? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa Serikali ya CCM ina malengo mema ya kuzalisha wahitimu mahiri wa masomo ya sayansi na wananchi wa Kata ya Kikatiti katika Wilaya ya Meru wamejitolea ujenzi wa maabara katika Shule ya Ngyeku Sekondari. Je, Serikali itawasaidiia wananchi hawa kumaliza maabara hii lini? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zaytun Swai.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge kwa maana amekuwa mstari wa mbele katika ufuatiliaji wa fedha hizi kuweza kupelekwa katika Mkoa wa Arusha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la kwanza, Serikali kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi ilianza na phase one ya shule 10 za mwanzo ambapo bilioni 30 zilitumika, kwa sasa katika mwaka huu wa fedha ambao tupo 2022/2023 tunaenda kwenye phase two ambapo disbursement ya shule tisa, fedha za shule tisa, itafanyika muda si mrefu ikiwemo ya Shule ya Arusha ambayo wao wenyewe wamepanga kuijenga kule Longido.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, kama nilivyosema hapo awali kwenye majibu mengine, Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI, inafanya tathmini kwa ajili ya maboma haya yakiwemo haya ambayo yapo kule kwenye Kata ya Kikatiti katika Shule hii ya Ngyeku kwa ajili ya kuona ni uhitaji wa fedha kiasi gani ambao tunao ili baadaye tuweze kukaa na wenzetu wa Wizara ya Fedha na kuomba fedha hizi kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma haya.