Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 607 2023-06-13

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza:-

Je lini Serikali itajenga barabara ya mchepuko kutoka barabara ya Tanga - Horohoro - Chongoleani?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwanaisha Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii inachepuka kutoka barabara ya Tanga - Horohoro kuelekea eneo ambalo kutajengwa bohari kubwa (depot) ya kupokelea mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia mradi huu wa bomba la mafuta na ujenzi wa bohari kwa ajili ya upokeaji wa mafuta unaofanywa na Kampuni ya EACOP ambao ndiyo wasimamizi wa mradi huu, waliomba kibali cha kuimarisha barabara ya Chongoleani kwa viwango ambavyo vitaweza kuhimili uzito wa magari na mitambo itakayokuwa inapitishwa katika barabara hii kwa kipindi chote cha ujenzi wa mradi hadi utakapokamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo kutokana na hali hiyo kwa sasa barabara hii inahudumiwa na EACOP kupitia Mkandarasi walieingia naye mkataba kwa kipindi chote cha mradi.