Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza:- Je lini Serikali itajenga barabara ya mchepuko kutoka barabara ya Tanga - Horohoro - Chongoleani?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Kwa kuwa, barabara ile ni ya changarawe na magari yenye uzito mkubwa ndiyo yanapita kuelekea kule kwenye matanki ya mafuta yanapojengwa na gharama ya kurudishia changarawe imekuwa ni kila baada ya miezi miwili ambayo inapelekea maintenance cost kuwa kubwa. Je, hamuoni haja kuishauri EACOP barabara ile ijengwe kwa kiwango cha lami kupunguza maintenance cost na kuweza kutumika baada ya mradi kukamilika? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Engineer Ulenge, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi kwamba barabara hii tayari baada ya utiwaji saini wa mkataba wa bomba la mafuta la Hoima tayari imehama kutoka TARURA na sasa inawahudumiwa na wao wenyewe EACOP. Tayari wameshaingia mkataba na mkandarasi wa kwao ambaye ataihudumia mpaka pale mradi huu utakapokamilika. Tunapokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge na tutaufanyia kazi kupitia wenzetu wa TARURA, kuweza kukaa na wenzetu wale wa EACOP kuona ni namna gani wanaweza kuanza walau taratibu kui - upgrade barabara hii lakini haya yote yanategemeana na uwepo wa fedha.