Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 608 2023-06-13

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza:¬-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha kikundi maalum kuweza kutathmini hewa ukaa?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, Mbunge Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kusini Pemba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tayari imeshaweka mipango thabiti ya kusimamia na kutathimini hewa ukaa. Ofisi ya Makamu wa Rais, imetoa Mamlaka kwa Kituo cha Uratibu na Usimamizi wa Kaboni (NCMC) kilichopo Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) kwa ajili kuratibu, kutathmini na kutoa utaalam wa masuala yote yanayohusu gesijoto na biashara ya hewa ukaa nchini. Aidha, katika kuhakikisha biashara ya hewa ukaa inakuwa biashara rasmi hapa nchini, Ofisi ya Makamu wa Rais, imeandaa kanuni na mwongozo wa kusimamia na kudhibiti biashara ya kaboni za mwaka 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Makamu wa Rais inaendelea kushirikiana na wadau wengine kwa kuhakikisha kwamba masuala haya ya hewa ukaa yanaeleweka kwa kila mdau na Watanzania wote kwa ujumla. Nakushukuru.