Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza:¬- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha kikundi maalum kuweza kutathmini hewa ukaa?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tayari Wizara imeshatunga katika kanuni na miongozo ya biashara ya hewa ukaa. Je, ni jitihada gani ya Wizara katika kutoa uelewa wa biashara hii kwa jamii hasa wanawake? (Makofi)

Swali langu la pili, je, Zanzibar inanufaika vipi kutokana na fedha inayotokana na faida ya biashara hii ya hewa ya ukaa? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, najibu maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Maryam pamoja na Wabunge wote kwa kuwa na hamu sana ya kutaka kujua faida na fursa mbalimbali ambazo zinapatikana kwenye biashara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Zanzibar sasa muda wowote inakwenda kuanza kunufaika kutoka na biashara hii, tulichokuwa sasa tunakisubiria ni kwanza tunasubiri tumalize utafiti. Zanzibar tunayo misitu kwa upande wa Pemba tunao Msitu wa Ngezi lakini kwa upande wa Unguja tunao Msitu wa Jozani na kama unavyojua kwamba biashara hii inavunwa kwenye misitu hasa misitu ya asili. Kwa hiyo, tutakapokamilisha utafiti wetu Zanzibar inakwenda kunufaika kwa kiasi kikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa tulisema wacha tuendelee kutoa taaluma kwa wananchi hasa kwa upande wa Zanzibar, tumeshaanza kushirikiana idara ya mazingira tumeanza kutoa taaluma, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi tumeanza kuwapa taaluma. Kwa hiyo, muda wowote kuanzia sasa Zanzibar inakwenda kuanza kunufaika na biashara hii ya hewa ukaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa jitihada ambazo zimechukuliwa ni kwamba, tumeunda kikosi kazi na kikosi kazi hichi kimekuwa kinashirikiana na TAMISEMI katika kuzunguka nchi yote kuhakikisha kwamba tunawafundisha wananchi. Tayari tumeshaanza kwenye baadhi ya Halmashauri za Mkoa wa Tabora, Simiyu, Katavi, Manyara na maeneo mengine. Kwa hiyo, taaluma hii tutahakikisha kwamba inaenea kote na juzi tulikuwa na Kamati za Wabunge kuwapa taaluma hii ya biashara ya hewa ukaa. Nakushukuru. (Makofi)