Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 609 2023-06-13

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza:-

Je, baada ya kuporomoka kwa bei ya korosho katika msimu wa 2022/2023 Serikali imechukua hatua gani kuhakikisha hali hiyo haijirudii?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, bei ya korosho Nchini hutegemea mwenendo wa bei katika Soko la Dunia. Mabadiliko ya mwenendo wa bei katika masoko hayo huchochewa na kiasi cha korosho kinachozalishwa Duniani na mahitaji kwa wakati husika. Kwa wastani katika msimu wa mwaka 2022/2023 bei ilishuka kutoka shilingi 2,150 hadi shilingi 1,850 kwa kilo kwa korosho daraja la kwanza na shilingi 1,595 hadi shilingi 1,332 kwa korosho daraja la pili.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi imeendelea na jitihada za kuimarisha bei ya korosho nchini kwa kufufua viwanda vya kubangua korosho pamoja na kuanzisha viwanda vipya. Vilevile, Serikali itaanzisha kongani la viwanda vya kubangua korosho ili kuongeza thamani ya korosho na kuuza moja kwa moja katika nchi walaji badala ya kuuza korosho ghafi.