Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza:- Je, baada ya kuporomoka kwa bei ya korosho katika msimu wa 2022/2023 Serikali imechukua hatua gani kuhakikisha hali hiyo haijirudii?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu lakini ninayo maswali mawili kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Lulindi ni mzalishaji mkubwa wa malighafi hya hivyo viwanda wanavyoahidi kuvijenga. Je, Serikali itajenga viwanda vingapi kwenye Jimbo la Lulindi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo cha korosho, zao hili pekee yake ndiyo linalochangia mfuko wa kilimo. Je, Serikali haioni sababu ya kutumia kiasi cha pesa zilizoko katika mfuko huu kwa ajili ya kutengenezea bima ya bei ya korosho? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza nataka nikiri ni kweli eneo la Lulindi ni kati ya wazalishaji wakubwa wa korosho. Kwa kutambua hilo Serikali pamoja na sekta binafsi itaendelea kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kubangua korosho katika eneo hili la Lulindi ili wakulima wengi zaidi waweze kunufaika na hatua hii ya uchakataji wa korosho.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusu bima, tumeshafanya mazungumzo na Shirika la Bima la Taifa kwa ajili ya kuhakikisha ya kwamba wanaingia katika zao hili la korosho ili tuweze kumlinda mkulima pale bei inapoporomoka. Hivi sasa tupo katika hatua nzuri na baadhi ya maeneo tumeanza majaribio naamini itawafikia wakulima wengi zaidi na itakuwa ni mkombozi mkubwa kwa wakulima wa korosho nchini Tanzania.