Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 613 2023-06-13

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itatenga fedha na kuanza ujenzi wa Mahakama ya Mkoa wa Songwe?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria naomba sasa nijibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwawa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe ulianza katika mwaka wa fedha 2021/2022, na jengo hilo lilijengwa eneo la Vwawa Wilayani Mbozi na lilikamilika Julai, 2022. Aidha, Jengo lilianza kutumika Agosti, 2022 na kuzinduliwa rasmi na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania mwezi Novemba, 2022 ambapo alizindua kwa pamoja na majengo ya Mahakama za Hakimu Mkazi katika Mikoa ya Lindi na Katavi, ahsante.