Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha na kuanza ujenzi wa Mahakama ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 1

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza naishukuru Serikali kwa kutenga fedha na kukamilisha hilo jengo.

Je, ni kwa kiwango gani jengo hili limekuwa jumuifu kwa maana ya kuwa na Mahakama ya Mwanzo, Mahakama ya Wilaya na Mahakama ya Mkoa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa kuna msongamano mkubwa sana katika Gereza la Ilembo pale Vwawa: Je, ni kwa kiwango gani jengo hili sasa litasaidia kuhakikisha kwamba kesi nyingi ambazo zimesongamana katika Mahakama zitaweza kwisha? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Naomba kujibu maswali mawili sasa ya Mheshimiwa Japhet, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza anataka kufahamu kama hili jengo litakuwa linajumuisha na Mahakama nyingine. Nimwarifu kwamba, katika mpango wetu wa Mahakama, miongoni mwa mikoa ambayo tunajenga majengo ambayo yatajumuisha Mahakama zote, ni pamoja na Mkoa wake. Kwa hiyo, hili limezingatiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, anataka kufahamu kama sasa kesi zitakwenda kwa kasi. Ni dhahiri kwamba kesi zitakwenda kwa kasi kwa sababu jengo hili baada ya kukamilika, efficiency ya Waheshimiwa Mahakimu wetu itaongezeka. (Makofi)

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha na kuanza ujenzi wa Mahakama ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 2

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama katika Wilaya ya Kiteto na Wilaya ya Hanang’ Mkoani Manyara?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Regina Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mahakama yetu ina mpango wa kujenga majengo yote ya Mahakama za Wilaya na za Mwanzo katika mikoa yote Tanzania. Katika mwaka wa fedha wa 2024/2025 tuna mpango wa kujenga Hanang’ pamoja na Kiteto. Kwa hiyo, Mahakama hizi ziko kwenye mpango. (Makofi)