Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 614 2023-06-13

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-

Je, kuna mpango gani kuvuna/kuwahamisha Tembo kutoka katika Pori la Rungwa, Muhesi na Kizigo ambao wanaingia katika Vijiji?

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inakiri kuwepo kwa changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu wakiwemo tembo. Kwa sasa Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Udhibiti Wanyamapori Wakali na Waharibifu wa Mwaka 2020/2024. Wizara inaendelea kufanya yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, ni kutoa elimu juu ya kujikinga na wanyamapori wakali na waharibifu; pili, kujenga vituo vya askari wanyamapori ili kusogeza huduma karibu na wananchi; na zaidi ya hapo ni kufunga mikanda (GPS collars) tembo kwa kuanzisha timu maalum.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuwashirikisha wananchi kwa kutoa mafunzo kwa askari wa vijiji ili kuongeza nguvu ya kudhibiti tembo katika maeneo ya wananchi, nakushukuru.