Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Je, kuna mpango gani kuvuna/kuwahamisha Tembo kutoka katika Pori la Rungwa, Muhesi na Kizigo ambao wanaingia katika Vijiji?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwa kuwa wanyama hawa wamekuwa wanashambulia watu na tatizo ni upungufu wa Askari: Je, ni lini Serikali itaongeza askari katika Kituo cha Doroto ambacho ni Makao Makuu ya Game Reserve ya Muhesi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kuna waathirika wengi wamevamiwa, wengine wameuawa, mashamba yao yameliwa na tembo, au wanyama wakali wameuawa: Je, ni lini mtalipa watu wetu hawa katika Jimbo langu katika Halmashauri ya Itigi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, najibu maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunakiri kwamba kuna upungufu wa askari ambao wanatakiwa walinde kwenye maeneo haya. Nimwambie tu Mheshimiwa kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, ndani ya mwezi huu tutahakikisha kwamba tunapeleka Askari katika kituo cha Doroto ili kuhakikisha kwamba shughuli za ulinzi wa wananchi dhidi ya wanyama wakali zinaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie tu kwamba tayari Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan imeshaachia kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wote walioathirika na athari za wanyamapori wakiwemo tembo wanapatiwa fidia zao na kupatiwa malipo yao, nakushukuru.

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Je, kuna mpango gani kuvuna/kuwahamisha Tembo kutoka katika Pori la Rungwa, Muhesi na Kizigo ambao wanaingia katika Vijiji?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la nyani na ngedere ambao wamekuwa ni waharibifu sana kwa mazao ya wananchi: Je, Serikali haioni sababu ya kuwahamisha au kuwauza nje ya nchi ili kujipatia fedha za kigeni? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya miongoni mwa wanyamapori ambao tunawatumia sana kwa shughuli zetu za utalii na kivutio cha watalii kwa ajili ya kuingiza mapato katika nchi yetu ni hao kima na wengine. Hata ukiangalia kwa mfano kwa upande wa Zanzibar, kule kuna wale kima ambao nadhani dunia nzima wanapatikana tu Zanzibar. Kwa hiyo, kwa kusema kwamba tuwachukue tuwasafirishe nadhani hili tulichukue tuende tukalifanyie kazi tukafikirie zaidi. (Makofi)