Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 616 2023-06-13

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza:-

Je, kuna mkakati gani wa kuhakikisha fedha za ujenzi wa Balozi za Tanzania zinapelekwa ili kupunguza gharama kubwa ya kodi?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felista Njau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, inatekeleza mpango mkakati wa miaka 15 wa kujenga, kununua na kukarabati majengo balozini kwa kipindi cha mwaka 2017/2018 hadi 2031/2032.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha Mwaka 2017/2018 na 2022/2023 Serikali imeweza kupeleka kiasi cha shilingi 10,357,785,067kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa majengo katika Balozi zetu nje ya nchi ili kuyaweka katika hali nzuri na hivyo kuipunguzia Serikali gharama kubwa ya kupanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Serikali imekamilisha uchambuzi na utekelezaji wa mpango huo na kuandaa mkakati wa utekelezaji ambapo jumla ya miradi 14 ya kipaumbele imeainishwa kutekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano cha mwaka 2022/2023 hadi 2026/2027 kupitia fedha za Serikali pamoja na ubia na sekta binafsi. Aidha, Serikali itaendelea kupeleka fedha za ujenzi na ukarabati wa majengo katika Balozi zetu kwa kadri hali ya upatikanaji wa fedha itakavyoruhusu, ahsante sana.