Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza:- Je, kuna mkakati gani wa kuhakikisha fedha za ujenzi wa Balozi za Tanzania zinapelekwa ili kupunguza gharama kubwa ya kodi?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa ujenzi wa balozi zetu nje ya nchi inachukua gharama kubwa ukilinganisha na hapa kwetu, lakini kikubwa kabisa bajeti ambayo tunaiweka kila mwaka haiwezi kuakisi ujenzi wa majengo hayo kutokana na kwamba itachukua muda mrefu na hatuwezi kuona tija: Serikali haioni sasa ni bora kuchukua mkopo katika taasisi za fedha nje au ndani ya nchi ili kujenga majengo hayo kwa mara moja ili kuleta tija? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Ujenzi wa balozi zetu unaleta tija kwenye Sekta ya Utalii, Biashara na Uwekezaji na huweza kuiletea Serikali pato la Taifa: Serikali haioni sasa ni bora kuainisha balozi za kimkakati ambazo zitaanza kujengwa mara moja ili kuletea Serikali yetu tija? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuanza na suala la kwanza, haya pia ni maelekezo mahususi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa makao makuu ya Benki ya CRDB mwaka 2022 kwa jinsi ni namna gani itumie taasisi binafsi na taasisi za fedha katika kuendeleza majengo yetu ubalozini. Hivi sasa tayari Serikali imeanza mazungumzo na Benki za CRDB na NMB pia na mifuko ya hifadhi ya jamii kama vile PSSSF, WCF na ICCF ili kuona vipi tunaweza kushirikiana katika suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la pili la kuainisha balozi za kimkakati. Huu ni ushauri mzuri sana wa Mheshimiwa Mbunge na tayari Serikali imeshaanza kutekeleza mkakati huo na kwa kuanzia tutaanzia na Ubalozi wa Nairobi, New York, Washington pamoja na Ubalozi wetu wa London, ahsante sana. (Makofi)