Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 49 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 638 2023-06-15

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa sekta ya afya kufikia asilimia 50 ya mahitaji katika Halmashauri ya Mbinga?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mahitaji makubwa ya watumishi wa afya katika Mamlaka za Serikali za Mitaa yaliyosababishwa na maboresho ya miundombinu yaliyofanyika katika ngazi ya afya ya Msingi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 na 2022/2023 Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ilipata kibali cha ajira na kuajiri watumishi wa kada ya afya 12,653 ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imepangiwa watumishi 68.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa kada ya afya kadri Bajeti ya Serikali itavyoruhusu.