Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa sekta ya afya kufikia asilimia 50 ya mahitaji katika Halmashauri ya Mbinga?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwanza niishukuru Serikali kwa kutoa watumishi hao 68. Lakini sasa kutokana na ongezeko hili kubwa la ujenzi wa vituo vya afya, ambapo tuna vituo viwili tayari vimekamilika, Kituo Cha Afya cha Mkumbi na Kituo cha Afya Matili, pamoja na ongezeko hili havijapata watumishi;

Je, ni nini kauli ya Serikali?

Mheshimiwa Spika, kutokana na upungufu uliopo Serikali iko tayari kuipa kipaumbele halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kutokana na upungufu Mkubwa uliopo wa watumishi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nijibu maswali mawili ya myongeza ya Mheshimiwa Benaya Kapinga. Kwanza hili la vituo viwili vya afya ambavyo vimejengwa na havijapata watumishi, naomba nitumie Bunge lako Tukufu kumwelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kuweza kufika katika vituo hivi viwili vya afya ambavyo amevitaja Mheshimiwa Kapinga na kufanya tathimini yake na kuona ni namna gani ambavyo tunaweza tukafanya msawazo wa watumishi ndani ya Mkoa wa Ruvuma walau kuanza kupeleka watumishi wachache ili waanze kutoa huduma kwa wananchi wa maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la pili, Serikali itaweka kipaumbele cha kupeleka watumishi kwenye maeneo yenye upungufu mkubwa ikiwemo kule Mbinga Vijijini kwa Mheshimiwa Kapinga. Na Kadri tutakavyoendelea kluajiri basi tutaweka kipanumbele kwenye maeneo hayo.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa sekta ya afya kufikia asilimia 50 ya mahitaji katika Halmashauri ya Mbinga?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Jimbo la Mbulu vijijini tumepata vituo vya Afya vitatu na tuna upungufu wa watumishi. Je, ni lini mnatuletea watumishi hao?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) Mheshimiwa Spika, nijibu swali la Mheshimiwa Massay, hivi sasa Serikali imetoka kuajiri watumishi 8070 wa kada ya afya nchini kote katika mwaka huu wa fedha 2022/2023. Pia tumeweka kipaumbele katika maeneo yenye upungufu ikiwemo kule Jimboni Mbulu Vijijini. Hivyo, basi ni wajibu wao na Mkurugenzi kuhakikisha kwamba hawa watumishi watakaopelekwa katika halmashauri yao wapangiwe kwenye maeneo ambayo yana upungufu zaidi.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa sekta ya afya kufikia asilimia 50 ya mahitaji katika Halmashauri ya Mbinga?

Supplementary Question 3

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa sisi Namtumbo tuna vituo viwili vya afya ambavyo vimejengwa na viko mwishoni kabisa kukamilika;

Je, Serikali haioni iko haja sasa ya kuanza kutuletea vifaa tiba na watunishi ili iweze kuanza na majengo yale yasikae muda mrefu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) Mheshimiwa Spika, kama nilivyomjibu Mheshimiwa Kapinga kwa kumwelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, anapotembelea kule Mbinga vijijini basi afike kule Namtumbo kwa Mheshimiwa Vita Kawawa ili kufanya tathimini kwenye vituo hivi vya afya ambavyo amevitaja Mheshimiwa Kawawa na kuona ni namna gani Serikali inaweza ikapaleka watumishi pale. Vile vile katika mwaka huu wa fedha tunaouanza wa 2023/2024 kuna fedha iliyotengwa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kote nchini. Hivyo basi, tutaona ni namna gani vituo hivyo vya Namtumbo vinapata.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa sekta ya afya kufikia asilimia 50 ya mahitaji katika Halmashauri ya Mbinga?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Hospitali ya Mji wa Mafinga kutokana na sababu za kijiografia inahudumia zaidi ya halmashauri tano. Je, Serikali iko tayari kutufanyia upendeleo wa kipekee?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema awali kwamba Serikali imeajiri watumishi 8,070 wa kada ya afya kote nchini na muda sio mrefu wametoka kuchukua barua zao katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI na kuweza kuripoti katika maeneo ya kazi waliyopangiwa ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Mafinga. Hivyo basi, ni imani yangu kuwa halmashauri hii imepata watumishi hawa wa kada ya afya. Ni wajibu wa Mkurugenzi kuwapangia kule kwenye upungufu ikiwemo katika hospitali ya wilaya.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa sekta ya afya kufikia asilimia 50 ya mahitaji katika Halmashauri ya Mbinga?

Supplementary Question 5

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Vituo vya Afya vya Mwang’aranga, Mwigumbi na Ukenyenge ni vituo ambavyo vina upungufu mkubwa sana wa watumishi;

Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba inapeleka watumishi kwenye vituo hivyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, katika Vituo hivi vya Afya vya Mwang’aranga, Mwigumbi na hicho kingine alichokitaja Mheshimiwa Butondo, muda sio mrefu Serikali imetoka kuajiri watumishi wa kad ya afya, hivyo tutakwenda kuangalia na kuona ni wangapi wamepangiwa kwenda katika Halmashauri ya Shinyanga DC na kuweza kuona ni namna gani wanaweza wakapelekwa katika vituo vya afya alivyovitaja Mheshimiwa Butondo.