Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 49 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 641 2023-06-15

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuviwezesha Vikundi vya Wanawake vya Ufugaji Mkoani Tanga ili viweze kuongeza tija?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantum Mzamilu Zodo, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa Mwaka wa Fedha wa 2021/2022 na 2022/2023 hadi mwezi Machi, Halmashauri za Mkoa wa Tanga zimetoa mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri yenye thamani ya Shilingi Bilioni 4.56. Kati ya fedha hizo kiasi cha Shilingi Bilioni 1.82 zimekopeshwa kwenye vikundi vya wanawake vinavyojishughulisha na biashara ndogondogo pamoja na ufugaji.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mchanganuo huo hapo juu, vikundi vya Wanawake 102 vyenye wanufaika 875 vinavyojishughulisha na kazi za ufugaji wa mifugo ya aina mbalimbali vimekopeshwa kiasi cha Shilingi Milioni 575 na kuweza kutengeneza ajira zipatazo 253.