Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuviwezesha Vikundi vya Wanawake vya Ufugaji Mkoani Tanga ili viweze kuongeza tija?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kuuliza swali moja dogo la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali toka robo ya tatu imesitisha kutoa mikopo hii ya asilimia 10 mpaka sasa na kwa kuwa akina mama wanahangaika na mikopo ya kausha damu huko mitaani; je, ni lini sasa Serikali inakwenda kuanza kutoa mikopo hii ya asilimia 10?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali ilisitisha utoaji wa mikopo hii ili kufanya tathmini na mapitio ya namna ambavyo mikopo hii inatolewa na hili lilikuwa ni agizo la Kamati ya Kudumu ya Bunge lako tukufu ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Hivi sasa timu ile imeshaundwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tayari wameanza kufanya kazi ya kufanya mapitio na vilevile ilikuwa ni malekezo yake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha mapitio haya yanafanyika haraka ili fedha zile nyingi zisipotee pale mikopo inapotolewa. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, tayari tumeshatoa maelekezo kwa Wakuu wa Mikoa wote, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri. Kwa mujibu wa kifungu au Kanuni ya 24(2) ya kanuni za utoaji wa mikopo hii, tayari kila Halmashauri ina akaunti mahususi kabisa ya mikopo hii na tumewaelekeza hakuna kusimama katika kupeleka asilimia 10. Kwa hiyo hela zitapelekwa na pili utaratibu mpya utakapotangazwa, basi tutakuwa tuna hela tayari kwa ajili ya kupeleka kwenye huo utoaji wa mikopo.

Kwa hiyo, hawatakiwi kusimama, wanatakiwa kuendelea kuzitenga katika akaunti za mikopo. Kilichosimama tu ni ule utoaji kwenda katika vikundi vya wanufaika, nakushukuru.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuviwezesha Vikundi vya Wanawake vya Ufugaji Mkoani Tanga ili viweze kuongeza tija?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini Serikali sasa itapeleka vifaranga bora vya mbuzi, kuku na ng’ombe ili kuboresha mikopo hiyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutakaa na wenzetu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuweza kuona ni namna gani tunapata mbegu bora kwa ajili ya kupeleka kwenye vikundi hivi ili waweze kufanya ufugaji ambao una tija na ambao utawaongezea kipato vilevile.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuviwezesha Vikundi vya Wanawake vya Ufugaji Mkoani Tanga ili viweze kuongeza tija?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, Serikali itazingatia kuongeza umri wa vijana kutoka ile miaka ya awali 30 mpaka kufikia 45 kama tulivyopendekeza?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, umri ule wa vijana uliowekwa pale ni kwa mujibu wa miongozo ya kimataifa ambayo inataja umri wa vijana ni upi. Kwa hiyo sisi tunaendana na convention zile za kimataifa na mikataba ya kimataifa. Kwa hiyo umri wa vijana utabaki vilevile.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuviwezesha Vikundi vya Wanawake vya Ufugaji Mkoani Tanga ili viweze kuongeza tija?

Supplementary Question 4

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, tumeona changamoto kubwa kwenye suala zima la mikopo; je, Serikali iko tayari sasa kubadili mfumo wa mikopo badala ya kutoa fedha kwenda kuwapa huduma kama ni ufugaji wa kuku, Serikali ikaamua kuwanunulia kuku ikawapatia wana kikundi badala ya kuwapa fedha ambazo haziendi kutimiza malengo ya ule mkopo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, baada ya maelekezo yale ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kufanya mapitio ya utoaji wa mikopo hii ya asilimia kumi na maelekezo ya Kamati yako ya Bunge ya TAMISEMI, hivi ni vitu ambavyo vinaenda kuangaliwa na timu ile ambayo ameiteua Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI.