Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 49 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 462 2023-06-15

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:-

Je, nini mpango wa Serikali wa kuondoa magugu ambayo yanasababisha uchafuzi katika Ziwa Victoria?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, napenda kujibu swali wa Mheshimiwa Kabula Enock Shitobela, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ili kudhibiti magugu maji yasiendelee kuleta athari katika Ziwa Victoria, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali tangu mwanzoni mwa miaka ya tisini. Hatua hizo ni pamoja na:-

(i) Kutekeleza Mradi wa Hifadhi ya Mazingira katika Ziwa Victoria (Lake Victoria Environmental Management Project) ambao pamoja na mambo mengine ulitekeleza shughuli zilizolenga kudhibiti magugu maji kwa kutumia njia mbalimbali zikiwemo za kibaiolojia;

(ii) Kutoa elimu na kuwajengea uwezo wananchi wanaoishi karibu na Ziwa namna ya kujitolea katika kazi za kutokomeza na kuenea kwa magugu maji kila yanapojitokeza Ziwani; na

(iii) Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais imeandaa na inatekeleza Mkakati na Mpango Kazi wa Taifa wa Kukabiliana na Viumbe Vamizi wa mwaka 2019-2029 ambao unatoa mwongozo wa namna ya kuzuia kuingia na kuenea kwa viumbe vamizi na pia una mipango endelevu ya kushughulikia viumbe vamizi waliopo na wale wale wanaoweza kuingia.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea na juhudi hizi za kupambana na magugu maji katika Ziwa Victoria ili kudhibiti uhabirifu wa mazingira na athari zitokanazo na uharibifu huo nchini, nakushukuru.