Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:- Je, nini mpango wa Serikali wa kuondoa magugu ambayo yanasababisha uchafuzi katika Ziwa Victoria?

Supplementary Question 1

MHE. KABULA E. SHITOBELA; Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa Serikali imeshaandaa mkakati maalum wa kukabiliana na changamoto ya viumbe vamizi. Je, ni lini mkakati huu utaanza kufanya kazi rasmi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shitobela kuwa mkakati huu umeshaanza kufanya kazi na umeshaanza kufanya kazi takribani karibu miaka miwili nyuma iliyopita. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na Wizara nyingine za kisekta kama vile Wizara ya Maji, Wizara ya Kilimo lakini pia Wizara ya Mifugo na sisi Mazingira tumekuwa tukishirikiana kwa karibu sana.

Mheshimiwa Spika, kwanza tunashirikiana kwa ajili ya kutoa elimu na takribani vikundi 40 tumeshavipa taaluma namna bora ya kutumia ziwa hili na kupunguza huu ueneaji wa haya magugu maji.

Mheshimiwa Spika, kikubwa nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaendelea kutafuta fedha, lengo na madhumuni ikiwa ni kuhakikisha kwamba, tunapambana na hili jambo kwa sababu ni jambo ambalo Ziwa Victoria limeingiza nchi tatu au nchi nyingine.

Kwa hiyo, sisi huku tukiyakata kwa wenzetu yanaendelea kumea, kwa hiyo na mwisho wa siku yanarudi tena kwetu, lakini hata hivyo tunaendelea kupambana changamoto hii, nakushukuru.

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:- Je, nini mpango wa Serikali wa kuondoa magugu ambayo yanasababisha uchafuzi katika Ziwa Victoria?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kupata nafasi hii. Ziwa jipya lililoko Wilayani kwangu Mwanga mpakani na Kenya, upande wa Tanzania unakaribia kupotea kabisa kwa ajili ya magugu maji. Je, Serikali ina mpango gani wa kutekeleza ahadi yake ya kuondoa magugu maji katika Ziwa Jipe? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, azma ya Serikali hii ni kuhakikisha kwamba tunaondosha changamoto zote zinazogusa kwenye eneo la mazingira ikiwemo changamoto ya kuenea kwa magugu maji. Nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaendelea kuzitafuta fedha kokote ziliko ili kuhakikisha kwamba tunaondoa magugu maji katika maeneo yote. Pia nimwambie kwamba siyo hili tu, yapo maziwa mengi yana changamoto hii. Hivyo, nimwambie tu kwamba hata katika Ziwa Jipe tutahakikisha tunakwenda kuondosha kabisa changamoto ya magugu maji, nakushukuru.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:- Je, nini mpango wa Serikali wa kuondoa magugu ambayo yanasababisha uchafuzi katika Ziwa Victoria?

Supplementary Question 3

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona; je, Serikali ina mpango gani wa kuokoa Ziwa Basutu ambalo kwa sasa linaonekana limejaa mchanga na kusababisha maji kusambaa kwenda kwenye makazi ya watu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Ziwa hili limekuwa lina changamoto kubwa ya kuingia kwa mchanga ambao sasa unakwenda kuleta athari kubwa ya kimazingira. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge ni kwamba tumeshashirikiana na wenzetu wa halmashauri na baadhi ya taasisi nyingine kama ambavyo nimeanza kujibu awali, kuhakikisha kwamba kwanza tunaendelea kuwapa elimu wananchi, kwa sababu tuligundua kwamba changamoto hii ya uingiaji wa mchanga na hayo masuala ya magugu maji, mengi tukiwatizama changamoto za kimazingira zinasababishwa na wananchi wenyewe hasa kwenye shughuli zao za kibinadamu za kawaida. Nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba, awe na subra Serikali inakwenda kushughulikia hilo.

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:- Je, nini mpango wa Serikali wa kuondoa magugu ambayo yanasababisha uchafuzi katika Ziwa Victoria?

Supplementary Question 4

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Serikali ina mkakati gani wa kupambana na mimea vamizi nchi kavu na majini ikiwa Dodoma tayari tuna mmea vamizi ambao unaitwa Kongwa?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, moja miongoni mwa changamoto siziiti mpya, lakini miongoni mwa changamoto za kimazingira ambazo tuko nazo sasa hivi ni changamoto ya kuvamiwa na viumbe vamizi ikiwemo mimea na wadudu. Kwa hiyo, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, suala hili tumeliona na tumeshaanza kulifanyia utafiti kwa sababu tumegundua kuna baadhi ya mimea mingine ni vamizi lakini haina athari kimazingira. Kwa hiyo, kwa hii ambayo ni vamizi na ina athari kimazingira tutahakikisha kwamba tunakwenda kulishughulikia na tutalifanyia kazi katika mikoa yote kwa sababu siyo Dodoma tu hata mikoa mingine tumegundua ipo hiyo changamoto. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:- Je, nini mpango wa Serikali wa kuondoa magugu ambayo yanasababisha uchafuzi katika Ziwa Victoria?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kwa kuwa suala la magugu maji limekuwa ni tatizo kubwa, ni kwa nini Serikali isifanye utafiti kuona kama kuna eneo ambalo magugu maji haya yanayotumika kama raw material ili yaweze kuvunwa kirahisi zaidi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, jambo ambalo Mheshimiwa Mbunge amelishauri ni jambo jema na kwa sababu tumegundua kwamba hata nchi jirani wameshaanza hivyo na ndio maana unakuta changamoto ya kuenea kwa magugu maji inakuwa kubwa sababu sisi tukiyatoa, kwa wenzetu yanakuwepo na kwa sababu Ziwa ni moja yanarudi.

Mheshimiwa Spika, wenzetu Uganda wameshaanza kulifanyia hilo, wanatengeneza mikeka na mambo mengine na sisi tumo kwenye kufanya utafiti, nini ambacho tunaweza tukatengeneza. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutahakikisha na sisi tunatumia magugu maji kama raw material kwa ajili ya kuinua vipato vya wananchi, nakushukuru.