Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 49 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 643 2023-06-15

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti mabadiliko ya tabianchi ambayo yamekuwa tishio kwa usalama wa viumbe?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge Wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeandaa sera, mikakati na mipango ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi ambayo inatoa elimu na namna bora ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa wadau wote muhimu wakiwemo wananchi katika maeneo yote nchini.

Mheshimiwa Spika, wananchi wanahamasishwa kuacha shughuli zinazochangia uharibifu wa mazingira na kusababisha athari za mabadiliko ya tabianchi zikiwemo kukata miti ovyo, kuepuka kilimo kisichoendelevu katika vyanzo vya maji, kuepuka ufugaji unaoharibu mazingira pamoja na uvuvi haramu. Vilevile, Serikali inachukua hatua kwa kuanzisha na kutekeleza miradi ya kuzuia madhara ya mabadiliko ya tabianchi.

Mheshimiwa Spika, napenda kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge kuwa Serikali inaendelea kusimamia sera, mipango na mikakati ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi ambayo inapatikana kwenye tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (www.vpo.go.tz )

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.