Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 49 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 644 2023-06-15

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kuwasajili wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo vya kati kwenye utaratibu wa Bima ya NHIF?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy John Sabu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya imeanzisha mpango wa bima ya afya kwa wanafunzi wa ngazi zote kwa kuchangia shilingi 50,400 kwa mwaka ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma za matibabu wakiwa masomoni, likizo na wakati wa mafunzo kwa vitendo.

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Machi, 2023 mfuko umeshasajili jumla ya wanafunzi 342,933 ikiwemo wa Shule za Msingi, Sekondari, Vyuo vya Kati na Vyuo Vikuu. Zoezi hili la kusajili wanafunzi ni endelevu kupitia shule na vyuo.