Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kuwasajili wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo vya kati kwenye utaratibu wa Bima ya NHIF?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa zoezi hili ni endelevu, je, Serikali imejipangaje sasa kuhakikisha kwamba wanafunzi ambao hawajasajiliwa wanasajiliwa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Pili; kwa kuwa utekelezaji wa zoezi hili si kwa takwa ama kwa mujibu wa sheria. Je, Serikali sasa ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba sheria hii inawekwa kuhakikisha kwamba wanafunzi wote wanasajiliwa katika Bima ya Afya? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri.

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ni nini tutafanya ili kusajili wanafunzi wengi zaidi, kikubwa ni kuendelea kuhamasishana kuwaomba wakuu wa shule na wazazi kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu wote kwa pamoja tuone umuhimu wa watoto wetu kuwa na bima ya afya kwa sababu ugonjwa hauji kwa kusema, ugonjwa unakuja kwa ghafla na vizuri kujipanga wakati wote, hilo ni moja.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu mpango gani, kwa sababu hili suala haliko kisheria, tunafanya nini. Mheshimiwa Mbunge ni kwamba ndiyo maana Serikali ilikuja na Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote ili kulifanya hili jambo liwe sasa la kisheria. Kikubwa ambacho nawomba Watanzania, nawaomba ninyi Wabunge tuendelee kuelewa na kupigana kwa pamoja kuhakikisha Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote unarudi hapa ili tuweze kufanya hili suala la kisheria kwa sababu masuala ya afya ni muhimu na afya ni uchumi wa nchi. (Makofi)