Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 49 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 647 2023-06-15

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:-

Je, Serikali inaonaje ikapunguza au kuondoa nauli kwenye vivuko vyote nchini kwa watu wenye ulemavu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inafahamu kuwepo na Watu Wenye Ulemavu wa aina mbalimbali ambao wanatumia huduma za vivuko kote Nchini. Aidha, suala la kupunguza au kutolipa nauli kwenye vivuko halijatamkwa kwenye Sheria ya Leseni za Usafirishaji.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, suala la kupunguza au kuondoa nauli limekuwa likifanyika kwa Watu Wenye Ulemavu waliopo kwenye mazingira hatarishi katika vyombo mbalimbali ikiwemo usafiri wa vivuko. Hii imefanyika kupitia ofisi za Wakuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Maafisa Ustawi wa Jamii katika Halmashauri husika.

Mheshimiwa Spika, aidha, nichukue nafasi hii kuwaomba Waheshimiwa Wabunge kuendelea kuwaelimisha wananchi kuhusu utaratibu huu wa kupunguza au kuondoa nauli kwa Watu Wenye Ulemavu au wenye mahitaji maalum. Ahsante.