Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:- Je, Serikali inaonaje ikapunguza au kuondoa nauli kwenye vivuko vyote nchini kwa watu wenye ulemavu?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini kwa uhalisia hawa Maafisa Ustawi wanakua hawapo kwenye hivi vivuko wakati watu hawa wanatumia huduma hii. Nini kauli ya Serikali kwa vivuko vyote nchini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa suala hili halijatamkwa wazi kwenye Sheria ya Leseni za Usafirishaji Nchini. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba suala hili linatamkwa wazi kwenye Sheria hii ya Leseni za Usafirishaji Nchini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, ni kweli kwamba hatuwaweki watu wa ustawi wa jamii kwenye vivuko lakini tunachotaka wafanye ni kwamba waende kwenye ofisi za Wakuu wa Wilaya pamoja na ofisi za ustawi wa jamii ambapo wanapewa barua ama vibali kwamba waweze kusaidiwa kwa sababu hawana uwezo hivyo waweze kuvuka kwenye vivuko ama kutumia kwenye vivuko kwa kupunguziwa ama bila kulipa, ndiyo maana tumesema Waheshimiwa Wabunge waendelee pamoja na Wakuu wa Wilaya na watu wa ustawi kuwafahamisha watu wenye ulemavu ama mahitaji maalum kwenda kabla hajaanza safari basi apate kile kibali ama barua ambayo atakapofika kwenye kivuko husika hatabughudhiwa na hilo limekuwa likifanyika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kutamka kisheria, kulipa ama kutolipa kwa watu wenye ulemavu linategemea na uwezo. Watu Wenye Ulemavu, kuna ulemavu wa aina mbalimbali, wako wenye ulemavu ambao kimsingi wana uwezo nadhani hapa tunachoongela kupunguza ama kutolipa ni wale kabisa ambao wamethibitika hawana uwezo na ndiyo maana pengine wanatakiwa waende kwenye ofisi husika ambao watasema kweli huyu hana uwezo kwa hiyo hastahili kulipa, lakini wale wenye uwezo nadhana ndiyo maana sheria haikutungwa ili waweze kulipa.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo kama kutakuwa na umuhimu nadhani tunazo sekta mbalimbali ambazo zinashughulikia hawa Watu Wenye Ulemavu labda sasa litachukuliwa na Serikali liangaliwe kama kuna haja ya kulitungia sheria. Ahsante. (Makofi)

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:- Je, Serikali inaonaje ikapunguza au kuondoa nauli kwenye vivuko vyote nchini kwa watu wenye ulemavu?

Supplementary Question 2

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa watu wenye ulemavu kwanza kwa idadi siyo wengi, lakini wengi wao hupata changamoto hata ya kuwa na kipato: Ni kwa nini kusiwepo na tamko dhahiri kwamba kila mwenye ulemavu at least unaoonekana aweze kuvuka bure kwenye vivuko ili kuwapunguzia adha? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, nimesema watu wenye ulemavu wanatofautiana kwa kiasi kikubwa sana, na wapo watu wenye ulemavu ambao wana uwezo pengine kukuzidi hata wewe Mheshimiwa Mbunge. Sasa ukisema tu mtu mwenye ulemavu yeyote asilipe, nadhani pia tutakuwa hatuwatendei haki. Tumesema watu wenye ulemavu ambao kweli vyombo vinaweza vikatambua huyu hana uwezo kwa kweli, hao wanatakiwa wasaidiwe, ahsante.