Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 49 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 648 2023-06-15

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami kwa Barabara ya Mlowo - Utambili hadi Kamsamba?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami mwaka 2020. Aidha, Serikali imeanza kuijenga kwa awamu barabara hii ambapo imekamilisha ujenzi wa Daraja la Momba lenye urefu wa mita 80 na barabara za maingilio zenye urefu wa mita 950.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha ujao wa 2023/2024 barabara hii imetengewa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante.