Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami kwa Barabara ya Mlowo - Utambili hadi Kamsamba?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwanza naishukuru Serikali, imesikia kilio cha wananchi wa Mbozi na Momba kwa kutenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi huo.

Swali langu la kwanza; je, ni kilomita ngapi sasa Serikali itaanza kwa awamu hii?

Mheshimiwa Spika, pili; je, ni lini mchakato wa kumpata mkandarasi utaanza ili ujenzi uanze? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 147 kwa mwaka ujao wa fedha tumepanga kuanza kuijenga kilometa 50.

Swali lake la pili kuhusu ni lini tutaanza, barabara hii tutaanza kuijenga ama kutafuta mkandarasi tutakapoanza utekelezaji wa bajeti wa 2023/2024, na ndipo tutakapoanza kutekeleza mpango huu wa kuanza kuijenga hii barabara kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami kwa Barabara ya Mlowo - Utambili hadi Kamsamba?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa fursa hiyo. Kwanza tumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kukubali kuanza kusaini kesho barabara karibu nane kwa mfumo wa EPC and F, maana Bungeni hapa imezungumzwa muda mrefu kuhusu hilo suala; je, mara baada ya kutangaza habari ya kusaini hiyo kesho, ni lini ujenzi utaanza kwa barabara hizo ikiwemo Mafinga – Mgololo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza niseme, barabara ambazo tunategemea kutia sahihi ni barabara saba. Pengine tu nilijulishe Bunge hili kwamba kazi kubwa ambayo tulikuwa Mheshimiwa Rais anakwenda kuifanya ni kusaini mikataba ya hizi barabara zote saba ambazo tumeziongelea sana hapa za EPC + F na kazi hiyo itafanyika kesho hapa Dodoma Jakaya Kikwete. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu pengine Wabunge wengine hawajapata taarifa, tungetamani pia Wabunge wote ambao hizo barabara zinapita waweze kushuhudia kitu kikubwa ambacho kinafanyika kuanza kujenga hizo kilometa 2,035 kwa mpigo. Muda ungetosha ningeweza kuwakumbusha zile barabara lakini kwa sababu ya muda, ni hizo barabara zote saba ambazo kwa ruhusa yako labda niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge ni barabara ya Masasi – Nachingwea hadi Liwale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Ifakara – Lupilo – Malinyi – Kilosa – Kwa Mpepo hadi Lumecha Namtumbo, nyingine ni barabara ya Igawa – Mbeya Mjini – Songwe hadi Tunduma, barabara ya Kongwa – Kibaya – Orkesumet – Rosinyai hadi Arusha, barabara ya kutoka Karatu - Mbulu – Hydom – Sibiti – Lalago hadi Maswa na mwisho ni barabara ya Mafinga – Mtwango – Mgololo, ahsante. (Makofi)