Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 49 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 649 2023-06-15

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Babati Galapo hadi Orkesumeti kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania TANROADS, imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami mwezi Februari, 2023. Kwa sasa Serikali inaendelea na zoezi la kufanya uthamini wa mali za wananchi watakaoathirika na mradi lililoanza tarehe 5 Juni, 2023 na inatarajiwa kukamilika tarehe 5 Julai, 2023. Baada ya zoezi la uthamini kukamilika na waathirika kulipwa fidia, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, ahsante.