Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Babati Galapo hadi Orkesumeti kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali iko tayari kutenga fedha katika mwaka wa fedha wa 2024/2025 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Ni lini Serikali itasaini mkataba na wakandarasi kwa ajili ya ujenzi wa kilomita nane za barabara ya lami ya Dareda Center kwenda Dareda Mission ikiwa sehemu ya kwanza ya ujenzi wa barabara hiyo kutoka Dareda kwenda Dongobesh? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ndiyo inayounganisha Makao Makuu ya Mji wa Manyara, Babati na Wilaya mbili ya Kiteto na Simanjiro. Kwa hiyo, ni wazi kama tulivyosema kwenye mpango wetu kwamba tutaziunganisha hizo barabara kwa kiwango cha lami, kwa hiyo, naamini kwa mwaka wa fedha utakaokuja, hizi barabara zitaingia kwenye mpango na ndiyo maana sasa hivi tunakamilisha usanifu wa kina.

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Dareda – Dongobesh ambayo tutaijenga kwa kuanza na kilomita nane, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu za manunuzi zimekamilika na tunategemea pengine kabla ya tarehe 22 kama taratibu zitakwenda kama tulivyopanga, mkandarasi awe ameonyeshwa site kuanza ujenzi wa hizo kilomita nane, ahsante. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Babati Galapo hadi Orkesumeti kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imefanya mapinduzi makubwa ya kutumia utaratibu wa EPC + Financing na kesho inasainisha mikataba saba hiyo; je, ipo tayari kuifikiria barabara ya Makofia – Mlandizi – Mzenga – Mwanarumango kwenye utaratibu huo siku za usoni? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ni wazi kwamba hii barabara aliyoitaja tumekuwa tunaitengea bajeti na bado hatujakamilisha kulipa fidia hasa kwa kipande cha Makofia hadi Mlandizi, lakini mpango ni kuijenga hii barabara yote kwa kiwango cha lami. Sasa kama itaingia kwenye utaratibu wa kawaida ama utaratibu wa EPC + F itategemea na kipindi hicho ambapo sasa tutaanza kuijenga hiyo barabara.

Mheshimiwa Spika, wakati najibu barabara za EPC nilisahau pia kuwakumbusha watu wa kuanzia Handeni – Kiberashi – Kibaya – Kwamtoro hadi Singida, pia hiyo barabara itakuwepo kesho, ahsante. (Makofi)