Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 651 2023-06-19

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaongeza mafao kwa askari wastaafu?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii huongeza kiwango cha pensheni ya kila mwezi ya wastaafu mara baada ya kufanya tathmini na kujua uendelevu wake na uwezo wa kulipa mafao kwa wanachama wake. Tathmini hiyo hufanyika kila baada ya miaka mitatu kwa kipindi kifupi, miaka mitano kwa kipindi cha kati na miaka kumi kwa kipindi kirefu.

Mheshimiwa Spika, Kanuni ya Ulipaji Mafao Namba 11(1) za mwaka 2018 zinaelekeza Mfuko wa PSSSF kuongeza pensheni kwa kuzingatia mfumuko wa bei na uendelevu wa mfuko kila baada ya miaka mitatu. Hata hivyo, ninayo furaha kukuarifu na kuarifu Bunge lako tukufu kuwa hadi sasa wastaafu wote wa Serikali walishaboreshewa pensheni zao za kila mwezi ambapo kiwango cha chini ni shilingi 100,000 inaendelea kulipwa tofauti na hapo ilivyokuwa awali, ahsante.