Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza mafao kwa askari wastaafu?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia fursa ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri yanayoridhisha.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza; je, Serikali imejipangaje kuhusu kulipa mafao ya wastaafu ambao hawajapata mafao hayo nikitolea mfano Wafanyakazi wa Shirika la Ndege Tanzania?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, ni hatua gani mnachukua kwa waajiri ambao hawalipi michango ya wanachama kwa wakati? Ahsante. (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Malembeka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na malipo au ucheleweshaji wa mafao tayari kwenye hatua hiyo tumeshavuka. Mpaka sasa mifuko yetu PSSSF pamoja na NSSF tayari tumekwishakuanza utaratibu wa ulipaji kupitia mfumo wa teknolojia ya TEHAMA ambapo wanachama wote wanapewa hata taarifa sasa kupitia simu za mkononi au simu ya kiganjani na yeyote yule ambaye amekuwa amecheleweshewa kupata mafao yake tumekuwa tukichukua hatua hasa katika kuhakikisha kwamba tunapata nyaraka zao sahihi na kwa wakati ili waweze kuweza kulipwa.

Kwa hiyo, wachache sana ambao wanapata changamoto hizo kwa sasa na ikitokea changamoto hizo zinatokea tumekuwa tukiwaomba aidha kupitia Mheshimiwa Waziri ambaye alizunguka Mikoa karibia nchi nzima kwa kupitia kikanda kwenye majiji alikutana na wastaafu na tumekuwa tukipokea na tuna desk maalum la kupokea changamoto hizo. Kwa hiyo, kama zipo nimuombe Mheshimiwa Mbunge anifikishie ikiwa ni pamoja na za ATCL kwa taarifa tulizonazo ofisini tayari wapo walikwishakulipwa zaidi ya wafanyakazi 500 na wale wachache ambao walikuwa wana changamoto ilikuwa ni kuhusiana na taarifa sahihi hazikuweza kuwasilishwa ofisini ili waweze kulipwa. Kama watakuwa wamepata nyaraka na taarifa sahihi tuko tayari kuweza kuwalipa mafao yao.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la waajiri kutokuwasilisha michango kwa wakati. Mifuko hii inazo sheria ambayo inaianzisha na katika sheria hizi zinaeleza ni kosa kwa mwajiri kutokuwasilisha michango kwa wakati katika mifuko hii kwa ajili ya wanachama na ikitokea hivyo hata mahakamani Bunge lako tukufu lilitunga sheria hii kwa kujua umuhimu wa watu hawa ni katika mfumo wa summary suit. Kwa hiyo, unapelekwa mahakamani, hakuna kujitetea na tunachua hatua.

Kwa hiyo, kama kuna maeneo ambayo watakuwa wamechelewesha michango kwa kweli nitoe rai kupitia Bunge lako tukufu kwamba tunawataka waajiri wote nchini kutekeleza hilo, kupeleka michango kwa wakati ya wanachama ili wasisumbuke, lakini pia sisi pia kutupunguzia mashauri yaliopo mahakamani, mpaka sasa tuna mashauri zaidi ya 26 na tumechukua hatua, ahsante.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza mafao kwa askari wastaafu?

Supplementary Question 2

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante; kwa kuwa suala la wastaafu kama hilo liko sawasawa na walioko Zanzibar, je, Wizara yako inatoa faraja gani kwa wale walioko Zanzibar wanaokawia kupata mafao yao au hawapati kwa wakati?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shomar kama alivyoeleza kuhusiana na kwamba changamoto zilizo upande wa Bara ni sawa na zile zilizopo upande wa Zanzibar. Kwa kuwa hii ni Serikali ya Muungano na tunafanyakazi kwa collective responsibility ninaomba kulichukua swali hili na tutawasiliana na Mamlaka za Zanzibar ili kuhakikisha wastaafu wetu hawapati tabu baada ya kustaafu.

Mheshimiwa Spika, pia nilieleze Bunge lako tukufu kwamba nimechukua na kupokea mwongozo wako kuhusiana na changamoto ambazo wanazipata. Lakini pia nitumie nafasi hii kwa sababu tumeshachukua hatua sana kuhusiana na kuwapeleka mahakamani, wakati mwingine mashauri pengine yanachelewa na watu wetu wanazidi kuumia.

Sasa naomba nifanye hatua moja na kwa Mheshimiwa Waziri kama hatua tuliokwishakuichukua kama unaniruhusu nitaje namba ya simu ambayo wakituma ujumbe pale mara moja wanaweza kupata huduma, lakini pia tuna ma–desk yetu kwenye zile ofisi tumezi–establish sasa kwa ajili ya kuwapa huduma wastaafu wetu na ni kwa kupiga simu tu ama kwa kuwasiliana kupitia WhatsApp na tunachukua hatua hizi.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli tukifanya mzaha wa hawa wastaafu na changamoto ambazo zimekuwepo tutachukua hatua kwa mameneja wetu wa mikoa ili kama hawezi kuwahudumuia Watanzania basi waje wengine wanaoweza kuwahudumia na hili ni agizo langu kwa mikoa yote wahakikishe hakuna malalamiko ya wastaafu na mameneja tutawapima kwa kiwango cha wanaolalamika kuhusu wastaafu. (Makofi)

SPIKA: Haya watajie namba maana ikitajwa hapa itakuwa na uzito, watajie namba wastaafu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, namba ni 0715939902. Ni 0715 939902, ahsante.

Name

Tamima Haji Abass

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza mafao kwa askari wastaafu?

Supplementary Question 3

MHE. TAMIMA HAJI ABASS: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali imejipangaje kutoa uelewa kwa watumishi wanaotarajia kustaafu hasa kuhusu kikokotoo? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tamima kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tumeendelea kutoa elimu ya kuhusiana na kikokotoo na kwa msingi huo mifuko yetu imeshirikiana na Chama cha Waajiri (ATE) katika kutoa elimu, lakini pia Shirikisho la Wafanyakazi (TUCTA), lakini pia tumekuwa tukiwafikia hata kwenye makundi kulingana na kada zilizopo za ajira. Kwa hiyo, hata hao ambao ameeleza Mheshimiwa Mbunge tutawafikia na swali la utoaji wa elimu kuhusiana na kikokotoo ni endelevu ili waweze kuona faida ambayo wanaweza kuipata kutokana na kikokotoo hiki kipya, ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza mafao kwa askari wastaafu?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, wastaafu wengi wamekuwa wanapata adha ya kufanya uhakiki wa mara kwa mara kuthibitisha kwamba bado wako hai, proof of life na wanahitajika kwenda makao makuu ya Wilaya au ama katika taasisi ambazo walistaafu kwa ajili ya kwenda kufanya hiyo proof of life?

Je, ni mkakati gani ambao Serikali mtachukua kuhakikisha kwamba kunakuwa na mfumo wa kisasa wa kuweza kufanya hiyo proof of life badala ya usumbufu ambao unaendelea kwa hivi sasa? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndugulile kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kulikuwa na changamoto sana ya wastaafu wetu kwenda kuambiwa kwamba anaenda kuhakikiwa taarifa na kadhalika, lakini tuliliona hilo na tukaanzisha mfumo maalum wa kuwahitaji wao kuwa na namba zao za mawasiliano za kiganjani, lakini pia kuanzisha portal maalum ya kutoa taarifa za wanachama na hatua ya pili tuliyoichukua ni kwamba kuhakikisha sasa taarifa hizi zinaenda on monthly basis kuhakikisha kwamba taarifa zake kwa wakati wote zinapatikana kwa Mfumo wa TEHAMA. Kwa hiyo, tumejihimarisha kwenye TEHAMA na tunafanya vizuri na sasa tumekwishakuanza kuwahudumia vizuri, ahsante.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza mafao kwa askari wastaafu?

Supplementary Question 5

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Kwa kuwa wapo walimu ambao michango yao ilikuwa haikupelekwa na watumishi, lakini wakaambiwa wajilipie wenyewe, wamejilipia wenyewe, wana risiti mkononi, lakini marekebisho ya mafao yao hayakufanyika.

Je, nini kauli ya Serikali kuhusiana na walimu hao? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Kisangi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza kwa Mwanachama ambaye alikuwa amesajiliwa kihalali na sahihi kabisa, lakini pia kuna mwajiri ambaye alikuwa na wajibu wa kulipa michango hajatekeleza wajibu wake na badala yake mwanachama akalazimika kujichangia mwenyewe, hilo kwanza siyo sahihi na linahitaji ufuatiliaji.

Kwa hiyo, niombe nipate takwimu sahihi za wanachama hao ambao walifanya hivyo na bado pia hawajaweza kutendewa haki, tulichukue kama ofisi na kwenda kulifanyia kazi, kwa sababu sina takwimu sahihi nitaomba nipate majina lakini pia na takwimu zao ili niende nikafanye ushughulikiaji wa jambo hili, ahsante.