Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 657 2023-06-19

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza:-

Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Karatu – Mbulu – Singida kilometa 190?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Awack Tlemai, Mbunge wa Karatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Karatu – Mbulu – Singida ni sehemu ya barabara ya Karatu – Mbulu – Hydom – Sibiti River – Lalago – Maswa yenye urefu wa kilometa 389. Serikali imeanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii ambapo sehemu ya Mbulu – Garbabi kilometa 25 kazi zinaendelea, sehemu ya Labay – Hydom kilometa 25) mkataba wa ujenzi umesainiwa tarehe 19 Mei, 2023 na sehemu iliyobaki itajengwa kupitia Mpango wa EPC + F wa barabara ya Karatu – Mbulu – Hydom – Sibiti River – Lalago – Maswa ambapo mkandarasi amepatikana na mkataba wa kuanza ujenzi umesainiwa tarehe 16 Juni, 2023, ahsante. (Makofi)