Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Karatu – Mbulu – Singida kilometa 190?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Daniel Awack nashukuru sana Serikali kwa majibu yake mazuri, lakini nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, je, ni lini barabara ya kutoka Redio Habari Maalum kwenda Hospitali ya Wilaya ya Arumeru itajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja ya maeneo ambayo tunayafanyia kazi sana ni pamoja na kupeleka barabara za lami kwenye maeneo yanayotoa huduma za jamii kama hospitali.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara ya Ujenzi pamoja na wenzetu wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa tutashirikiana kuhakikisha kwamba hii barabara ambayo ni fupi sana kilometa tatu inafanyiwa usanifu na kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Karatu – Mbulu – Singida kilometa 190?

Supplementary Question 2

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa na mimi swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Magugu – Mbuyu wa Mjerumani – Mbulu ni barabara muhimu sana kwa wakazi wa Mbulu na Babati, lakini kipande cha Mbuyu wa Mjerumani – Mbulu ni hatarishi sana kwa kipindi cha mvua.

Sasa ni lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mbuyu wa Mjerumani – Daraja la Magala hadi Mbulu imeshakamilishwa kufanyiwa usanifu wa kina na tayari daraja tumeshajenga. Tunachofanya sasa hivi kwenye hii barabara ni kujenga kwa kiwango cha zege maeneo yote hatarishi na hasa kwenye escapement, lakini wakati huo tukiwa tunatafuta fedha kujenga barabara yote hii kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Karatu – Mbulu – Singida kilometa 190?

Supplementary Question 3

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Spika, barabara kutoka Mombo – Soni – Lushoto ni barabara nyembamba sana, ni mlimani, ni kona kali na imewekewa mpango kwa ajili ya kupanuliwa. Nataka kujua, je, mpango huo bado upo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nakiri na mimi nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara aliyotaja ya Mombo hadi Soni ni barabara ya lami ilijengwa zamani na ni nyembamba sana na ipo kwenye miinuko. Ni kweli kwamba Serikali ina mpango wa kuiboresha kwa maana ya kuipanua, kupunguza kona na kupunguza ile miinuko ili barabara hii iwe salama kwa watumiaji wote wanaoitumia kutoka Mombo kwenda Lushoto na Mlalo, ahsante. (Makofi)

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Karatu – Mbulu – Singida kilometa 190?

Supplementary Question 4

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, wananchi wa Jimbo la Kibaha Vijijini, Bagamoyo, Kibaha Mjini na Kisarawe wamepewa ahadi ya ujenzi wa barabara yao ya lami ya Makofia – Mlandizi – Kisarawe kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi hii inayoendelea.

Je, ni lini itaingia kwenye kusainiwa mikataba kama ilivyofanywa barabara za juzi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii ni muhimu sana kwa maendeleo yetu na hasa inayounganisha barabara ya Bagamoyo na hii barabara ya Morogoro. Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kitu cha kwanza ambacho kitafanyika kwanza ni kulipa fidia kwa wananchi ambao tayari walishaainishwa ili waweze kupisha barabara na tumetenga fedha kwa mwaka ujao kwa ajili ya kuanza hiyo barabara ya Makofia – Mlandizi kwenda Mzenga huko Kisarawe, ahsante. (Makofi)