Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 658 2023-06-19

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaendeleza barabara ya Mpanda - Kahama ili ifike Ulyankulu - Urambo - Ussoke - Tutuo - Sikonge hadi Mbeya?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANROADS inaendelea na kazi ya ujenzi wa barabara hizi kwa awamu kwa kiwango cha lami ambapo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya kutoka Mpanda – Ugalla – Kaliua – Ulyankulu hadi Kahama urefu wa kilometa 457 umekamilika na sehemu ya barabara kutoka Urambo hadi Ussoke kilometa 45 tayari imejengwa kwa kiwango cha lami. Kwa sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara za Ulyankulu hadi Urambo na Tutuo hadi Ussoke na baada ya kukamilika kwa usanifu huo Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hizi kwa kiwango cha lami, ahsante.