Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Je, lini Serikali itaendeleza barabara ya Mpanda - Kahama ili ifike Ulyankulu - Urambo - Ussoke - Tutuo - Sikonge hadi Mbeya?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kutokana na umuhimu wa barabara hiyo katika kuchochea uchumi wa wananchi wa Urambo, ni lini barabara hiyo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ikitokea Kahama – Ulyankulu – Urambo – Ussoke – Tutuo – Sikonge ili waendelee wasafiri mpaka Mbeya? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kadri tunavyofungua nchi na kuunganisha miji barabara aliyoitaja ni muhimu sana hasa kwa sababu itapunguza sana urefu wanaosafiri watu wa kutoka Kahama na hata watu wanaotoka njia ya Kigoma ambao kama wanaenda Mbeya hawana sababu ya kupita Mjini Tabora. Ndio maana tumesema tunaendelea kuhakikisha kwamba tunafanyia usanifu hiyo barabara ya kutoka Ulyankulu hadi Urambo na kipande cha Ussoke hadi Tutuo ili kuwapunguzia wananchi hawa umbali mrefu wa kusafiri.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kinachotakiwa sasahivi tunatafuta fedha sasa ili barabara hii ifanyiwe usanifu na ijengwe kwa kiwango cha lami kwa ajili ya kufungua hilo eneo la Wilaya ya Urambo, lakini pia na kuunganisha na Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Je, lini Serikali itaendeleza barabara ya Mpanda - Kahama ili ifike Ulyankulu - Urambo - Ussoke - Tutuo - Sikonge hadi Mbeya?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, barabara ya kutoka Mbamba Bay hadi Lituhi imo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi kujengwa kwa kiwango cha lami. Je, Serikali imefikia wapi katika suala hilo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, barabara aliyoitaja ina sifa mbili, kwanza ni barabara ya ulinzi lakini pia ni barabara ambayo inaambaa ambaa na ziwa kutoka Mbamba Bay kwenda Lituhi. Barabara hii tulishafanya usanifu na sasa kinachotafutwa ni fedha ili kuijenga kwa kiwango cha lami ambapo itaunganisha Bandari ya Mbamba Bay ambayo tayari kuna lami, lakini na Lituhi ambako sasa Mheshimiwa Mbunge anakubali tunajenga kuanzia Amani Makolo mpaka Bandari ya Ndumbi. Kwa hiyo, kipande kilichobaki hapo tukishaunganisha tutakuwa tumekamilisha barabara za lami na itakuwa ni rahisi sana kufanya ulinzi, lakini pia kufungua Wilaya ya Nyasa, ahsante.