Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Water and Irrigation Wizara ya Maji 661 2023-06-19

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA K.n.y. MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: -

Je, nini mpango wa kuweka miundombinu ya kuhifadhi maji ya mvua badala ya kusababisha mafuriko Kata za Loya na Miswaki?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilifanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa bwawa katika Kata ya Miswaki, lakini taarifa za kitaalam zilionesha eneo hilo kutokukidhi. Usanifu wa bwawa uliofanyika katika eneo la Kata ya Kizengi ulileta matokeo mazuri na Serikali inatarajia kuanza ujenzi wa bwawa katika mwaka wa fedha 2023/2024. Kukamilika kwa bwawa hilo kutaboresha huduma ya maji kwenye vijiji kumi vya Kata za Loya, Miswaki na Kizengi. Aidha, wananchi wanaofanya shughuli za kilimo maeneo ya mabondeni wanashauriwa kuhama kipindi cha mvua kubwa.