Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA K.n.y. MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, nini mpango wa kuweka miundombinu ya kuhifadhi maji ya mvua badala ya kusababisha mafuriko Kata za Loya na Miswaki?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwanza niishukuru Serikali kwa niaba ya wananchi wa Igalula kwa kuanza kujenga bwawa kwa ajili ya kutatua changamoto, lakini tatizo hili pia lipo Igunga kwenye Kata za Itumba, Lugubu na Nguvumoja. Maji yamekuwa yakijaa kwa sababu ule ni ukanda wa Bonde la Mbeya ambalo linakwenda mpaka Igalula.

Je, ni lini Serikali itafanya kwa wananchi wa Jimbo la Igunga katika kutatua changamoto hii? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nicholaus George Ngassa, Mbunge wa Jimbo la Igunga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nipende kupokea shukrani kwa Serikali kutekeleza wajibu wake, na kwa maeneo ya kata ulizozitaja kwenye Jimbo la Igunga Mheshimiwa Mbunge na yenyewe pia tutaendelea kuwaletea wataalam waweze kufanya usanifu na tuweze kuchimba mabwawa maeneo yote ambayo yatasaidia kuondosha na kupunguza mafuriko.

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA K.n.y. MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, nini mpango wa kuweka miundombinu ya kuhifadhi maji ya mvua badala ya kusababisha mafuriko Kata za Loya na Miswaki?

Supplementary Question 2

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru, katika Kata za Fukayosi na Makurunge katika Jimbo la Bagamoyo, DAWASA Chalinze wamesambaza miundombinu ya maji mwaka wa pili sasa lakini maji hayatoki.

Je, ni lini sasa maji katika maeneo haya yatatoka?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba niwe nimelipokea, nikalifanyie ufuatiliaji kwa nini maji hayatoki na usambazaji umefanyika.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA K.n.y. MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, nini mpango wa kuweka miundombinu ya kuhifadhi maji ya mvua badala ya kusababisha mafuriko Kata za Loya na Miswaki?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa tatizo la maji kutiririka hovyo wakati wa mvua ni tatizo kubwa sana kwa maeneo ambayo yako kwenye milima ukiwemo Mkoa wa Kilimanjaro.

Ni lini sasa Serikali italeta muswada hapa Bungeni ili nyumba zote zinazojengwa ziwekewe vikinga maji na kutumia maji yale ya mvua?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuleta muswada niseme nimelipokea, lakini sisi kama Wizara tayari tumejipanga na kuona kwamba mabwawa tutakayoyachimba tutaweka kwenye maeneo yote ambayo ni korofi kwa sasa, na tumshukuru Mheshimiwa Rais ameweza kutupatia vitendea kazi, tumeshanunua seti tano kwa ajili ya uchimbaji wa mabwawa.

Mheshimiwa Spika, lakini hilo aliloliongea Mheshimiwa Mbunge naomba niseme nimelipokea.