Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 50 Energy and Minerals Wizara ya Madini 662 2023-06-19

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza:-

Je, kuna mkakati gani wa kutatua kero zinazowakabili wachimbaji na wasafirishaji wadogo wa dhahabu Mgodi wa Kebaga?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Michael Mwita Kembaki, Mbunge wa Tarime Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Kebaga kilichopo Wilaya ya Tarime kina madini ya dhahabu ambayo wachimbaji wadogo wanachimba.

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wachimbaji hao wanafanya shughuli zao ipasavyo, Wizara kupitia Tume ya Madini imeanzisha kituo kidogo cha ununuzi wa dhahabu katika eneo la Kebaga ambapo wachimbaji huuza madini yao. Aidha, Tume ya Madini hufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa lengo la kuhakikisha wachimbaji na wachenjuaji wa dhahabu wanafanya kazi hizo kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Madini na kushughulikia kero zozote zinazowasilishwa na wachimbaji wa mgodi huo, ahsante sana.