Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza:- Je, kuna mkakati gani wa kutatua kero zinazowakabili wachimbaji na wasafirishaji wadogo wa dhahabu Mgodi wa Kebaga?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Mgodi wa Kebaga wachimbaji wadogo ambao wanachimba pale wanapata wakati mgumu wa kuuza dhahabu kwa sababu wataalam wanaokwenda kufanya tozo zile za dhahabu wanachelewa kwenda pale, hawana siku maalum ya kwenda kufanya tathmini.

Je, lini Serikali itaweka utaratibu mzuri wa siku zile za kwenda kuhakiki ili kutoa nafasi kwa wachimbaji wale kuuza madini yao? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, upo ushuru unaokusanywa pale na hakuna risiti za EFD ambazo zinatolewa, wanapewa risiti za kawaida; je, huu ni utaratibu ambao unakubalika na sheria?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kuhusu kuchelewa kununuliwa kwa madini ya wachimbaji wadogo, ninapenda kurejea majibu yangu ya msingi kwamba kwa kufahamu umuhimu wa shughuli za uchimbaji wa madini pale, tumeanzisha kituo kidogo cha ununuzi wa madini na mchimbaji yeyote ambaye ameshachimba madini yake akifika pale tathmini hufanyika na biashara hufanyika.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili kwamba kunakuwa na ucheleweshaji katika kuwahudumia hawa wachimbaji wadogo na wanatoa risiti ambazo ni za karatasi, kama changamoto hiyo ipo, nitamwomba Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi hiki tukutane na tuwasiliane na RMO kule tujue changamoto hiyo hutokana na nini ili tuweze kuishughulikia kikamilifu.