Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 57 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 749 2023-06-28

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kabla zahanati haijafunguliwa inawekewa vifaa tiba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Kainja Andrea, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni 15.15 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwenye zahanati ambazo zimekamilika ambapo tayari Serikali imekwishatoa fedha shilingi bilioni 12.90.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 Serikali imetenga fedha shilingi bilioni 18.4 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwenye zahanati zote zinazoendelea kukamilishwa na itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya zahanati zinazoendelea kukamilishwa kwa kadri fedha zinavyopatikana.