Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 57 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 751 2023-06-28

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: -

Je, lini Serikali itafanya marekebisho ya Sheria ya Usalama Barabarani ili kuweka tozo tofauti kulingana na ukubwa wa chombo cha moto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kufanya marekebisho na kuiboresha Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168 ya mwaka 1973 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002. Kwa sasa Serikali inaendelea kuboresha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Usalama Barabarani ambao tayari ulishasomwa kwa mara ya kwanza hapa Bungeni. Pamoja na mambo mengine, mswada huo umezingatia mahitaji ya sasa ikiwa ni pamoja na kuweka viwango tofauti vya tozo kulingana na ukubwa wa chombo cha moto kama Mheshimiwa Mbunge anavyoshauri, nashukuru.