Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 737 2023-06-27

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kubadilisha Mfumo wa Uandaaji Mpango wa Bajeti ili uwe wa zaidi ya miaka mitano?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali unaongozwa na Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025 ambapo katika kutekeleza malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, Serikali iliandaa Mpango Elekezi wa Muda Mrefu wa miaka 15 kuanzia 2011/2012 hadi 2025/2026 uliogawanywa katika vipindi vitatu vya muda wa kati wa miaka mitano ya utekelezaji (Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa Taifa 2011/2012 hadi 2015/2016, Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa 2016/2017 hadi 2020/2021 na Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa 2021/2022 hadi 2025/2026.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mfumo wa uuandaji wa mpango na bajeti wenye kutoa mwelekeo wa zaidi ya miaka mitano ambapo mpango na bajeti unaoandaliwa kila mwaka ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Maendeleo na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, ahsante.