Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kubadilisha Mfumo wa Uandaaji Mpango wa Bajeti ili uwe wa zaidi ya miaka mitano?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tayari sasa Serikali imeshazindua Tume ya Mipango ya Taifa, je, Serikali haioni ni wakati sahihi sasa kuwa na mipango ya miaka 100 na kuendelea ya Taifa letu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, je, Serikali haioni ni wakati sahihi sasa kuanza kuwa na mpango wa maendeleo wa miaka 100 na kuanza kuitekeleza kwa kipindi cha miaka mitano mitano?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa ridhaa yako naomba nijibu kwa pamoja. Ni jambo zuri kuwa na mpango wa muda mrefu sana wa hiyo miaka 100 au zaidi ya hapo lakini kwa kuwa Tume ya Mipango imeshaanzishwa au inaendelea kuanzishwa kwa sasa, huko siku za mbeleni tutaangalia suala hilo. Serikali imechukua shauri hilo na litafanyiwa kazi kadiri uwezekano utakapopatikana ikionekana kama iko tija. Kwa kuwa tayari sasa hivi tupo tunaandaa Dira ya Taifa 2050 itakayoanzwa kutekelezwa mwaka 2026 mara tu Dira ya 2025 itakapohitimishwa, ahsante.