Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 56 Water and Irrigation Wizara ya Maji 738 2023-06-27

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Mradi wa Maji wa Tarafa ya Suba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Jimbo la Rorya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Tarafa ya Suba ina vijiji 17 ambapo kati yake vijiji 16 vinapata huduma ya maji kupitia Vyanzo vya Ziwa Victoria, visima virefu na visima vifupi. Hata hivyo, kulingana na jiografia sio vitongoji vyote kwenye vijiji hivyo vinafikiwa na huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi wa vijiji hivyo 16 wanapata huduma ya maji salama na ya kutosheleza ikiwemo Wananchi wa Kijiji cha Kibui ambacho wananchi wake hawana maji, Serikali katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 itafanya usanifu wa mradi wa kutoa maji kwenye bomba kuu litakalopeleka maji Miji ya Tarime na Rorya ili kupeleka maji Vijiji vya Tarafa ya Suba. Baada ya kujengwa kwa mradi huo wananchi wote katika Tarafa ya Suba watapata huduma ya majisafi, salama na ya kutosheleza.