Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Mradi wa Maji wa Tarafa ya Suba?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, pamoja na majibu mazuri na kazi nzuri inayofanywa na Wizara hii kwa maana ya Naibu Waziri na Mheshimiwa Waziri, ninayo maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Tarafa ya Suba yeye vijiji 20 na sio 17 vijiji vinne kwa maana ya Kijiji cha Ruhu, Muundwe, Kibuyu na Mkengwa ni vijiji ambavyo havina mradi wowote wa maji mpaka sasa. Ninataka nipate kauli ya Serikali juu ya vijiji ni lini sasa vitapata maji safi na salama?

Mheshimiwa Spika, lakini swali langu la pili, pamoja na vijiji 16 kuwa na maji safi na salama lakini vitongoji katika vijiji hivi maji hayajatapakaa kwenye vitongoji. Nayo pia nilitaka nipate kauli ya Serikali, kwamba Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuhakikisha angalau vitongoji kwenye vijiji hivi 16 vinapata maji safi na salama kwa ajili ya huduma ya maji kwa wananchi hao?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chege kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, awali ya yote niseme nimepokea marekebisho ya idadi ya vijiji vyake lakini vilevile katika maeneo haya aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge nipende kumuelekeza Meneja wa Wilaya aendelee kufanya jitihada za kuona anapata visima ili vijiji hivi vipate maji. Mheshimiwa Mbunge eneo lako ni moja ya maeneo yanayonufaika na mradi ya miji 28. Kwa hiyo, wakati miji 28 utekelezaji unaendelea na ni kwa sababu ni mradi wa muda mrefu, jitihada za miradi ya muda mfupi zitaendelea kufanyika na ushirikiano wako namna ambavyo umekuwa ukiufanya, tutahakikisha tunafanya yale tuliokubalina.

Mheshimiwa Spika, katika vijiji hivi 16, vitongoji ambavyo havina maji tutahakikisha tunasambaza maji, Meneja wa Wilaya tayari tumemuelekeza na ninamsisitiza ili ahakikishe maeneo yote yanapata maji safi na salama. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Mradi wa Maji wa Tarafa ya Suba?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Mpango wa kutekeleza mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Kata za Magata, Muleba, Buleza, Chikuku na Kagoma utaanza lini? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Kagera, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, maeneo haya aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge Oliver, kwanza tulishakaana naye ofisini na tulishamwelekeza. Mheshimiwa Mbunge nakupongeza kwa ufuatiliaji, hizi kata ulizozitaja kama tulivyokubaliana ni lazima mwaka ujao wa fedha tuhakikishe na zenyewe zinakwenda kupata maji safi na salama. (Makofi)